Monday, November 10, 2014

Wanandoa wauawa kwa kukatwa vichwa



Na Mwandishi wetu

Wanandoa wawili wameuawa kwa kukatwakatwa mapanga na kutenganishwa vichwa na viwiliwili vyao.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Kagera, Henry Mwaimbambe alisema jana kuwa mauaji hayo yalitokea Novemba 7, mwaka huu saa 2.30 usiku nyumbani kwa wanandoa hao kata ya Nshamba, wilayani Muleba.

Kamanda Mwaibambe aliwataja marehemu hao kuwa ni Alhaji Sadick Hamisi(84) na Zamda Sadick(44).

Alisema wakati wanandoa hao walipokuwa wakijiandaa kupata chakula cha usiku watu wasiojulikana waliwagongea na kuwataka wafungue mlango.
Kamanda huyo alisema mlango ulipofunguliwa watu hao waliwashambulia wanandoa hao na kuwaua.

Alisema mtoto mmoja wa marehemu anashikiliwa na polisi akituhumiwa kuhusika na mauaji hayo.

No comments: