Tuesday, November 18, 2014

Mzumbe kumuenzi Nyerere leo

Na Mwandishi wetu, Morogoro
Chuo Kikuu Mzumbe leo kinaendesha warsha ya kumuenzi baba wa Taifa, Mwalimu Julius K. Nyerere.

Warsha hii ni mfululizo wa utaratibu ambao chuo hicho kimejiwekea ambapo kila mwaka mada mbalimbali huwasilishwa na wasomi na kujadiliwa ili kuenzi maisha ya baba wa Taifa na kuchangia mawazo ya maendeleo.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Mawasiliano, Chuo Kikuu Mzumbe, Bi. Rainfrida Ngatunga, mgeni rasmi katika warsha hiyo anatarajiwa kuwa mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dk. Joel Bendera.

Mada kuu ni mtazamo wa Mwalimu kuhusu katiba kama chombo cha kujenga demokgrasia.

Kongamano hilo linafanyika katika kampasi kuu ya chuo hicho mjini Morogoro.

“Mada mbalimbali zitajadiliwa msingi ukiwa kutoa mchango kwa maendeleo ya nchi yetu,” alisema Bi. Ngatunga.

Kwa mujibu wa Mkurungenzi huyo, wadau mbalimbali toka ndani na nje ya chuo hicho wanatarajiwa kuhudhuria warsha hiyo.


Mada zitawasilishwa na wanazuoni wa Mzumbe na toka nje ya chuo hicho.

No comments: