Friday, November 28, 2014

Tanzania yaongoza EAC kuvutia wawekezaji

Dar es Salaam
Tanzania ni nchi ya kwanza kwa Afrika Mashariki kaika kuvutia uwekezaji kutokana na sera iliyopo ikiwamo kudhibiti mfumuko wa bei.

Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Mwenyekiti wa Bodi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Umoja (UTT), Profesa Joseph Kuzilwa, wakati akifungua Mkutano mkuu wa tisa wa mwaka wa wawekezaji wa Mfuko wa Umoja.

Alisema mbali na Tanzania kushika nafasi ya kwanza, Pia ni ya nane kwa ukanda wa Jangwa la Sahara kwa uwekezaji.

Katika mkutano huo, Profesa Kuzilwa alisema mfuko huo umekua kwa kiwango cha asilimia 51.2 kutoka Sh 118.3 billioni mwaka 2012/13 hadi kufikia Sh 178.9 billioni mwaka huu.

“Idadi ya wawekezaji kwenye mfuko huu imeongezeka na kufikia 117,471 kwa mwaka wa fedha ulioshia Juni 30, mwaka huu na kwamba Mfuko wa Umoja pekee umeongezeka kwa kiwango cha asilimia 51.3 kutoka Sh 162.2 bilioni na wawekezaji kwenye mfuko huo walioongezeka kutoka 106,266 hadi 107,376,” alisema Profesa.


Aliitaja changamoto inayowakabili kuwa ni mabadiliko ya teknolojia yaliyosababisha meneja wa mfuko kuendelea kuwekeza katika tehama ili kuendana na ukuzaji wa soko na kufikia matarajio ya wawekezaji.

No comments: