Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) Bw. Raymond
Mbilinyi akisisitiza jambo wakati wa Mkutano wa Baraza la Biashara la Mkoa wa
Ruvuma hivi karibuni.Mkutano huo pamoja na mambo mengine ulijadili namna
ya kuweka mazingira wezeshi ya kufanya biashara na uwekezaji katika halmashauri
za mkoa huo, kujenga ushirikiano wa pande mbili kati ya sekta ya umma na
binafsi. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu na (katikati) ni
Mwenyekiti wa Chama cha wafanyabiashara wenye viwanda na kilimo mkoani humo(
TCCIA), Bw.Yohana Nchimbi, mkutano huo.
Baadhi ya wajumbe wa baraza la biashara la mkoa wa Ruvuma
wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zinatolewa Mkutano wa Baraza
la Biashara la Mkoa wa Ruvuma hivi karibuni.Mkutano huo pamoja na mambo mengine
ulijadili namna ya kuweka mazingira wezeshi ya kufanya biashara na
uwekezaji katika halmashauri za mkoa huo, kujenga ushirikiano wa pande mbili
kati ya sekta ya umma na binafsi
Na Mwandishi Wetu, Songea
Halmashauri mkoani Ruvuma
zimepewa changamoto kujitathimini kutokana na kuibua fursa za kibiashara na
uwekezaji zilizopo katika maeneo husika na kuzitangaza iliziweze kuwavutia
wawekezaji zaidi.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la
Biashara (TNBC) ,Bw. Raymond Mbilinyi alitoa wito huo kwa wajumbe wa Baraza la
Biashara la Mkoa wa Ruvuma hivi karibuni mjini hapa kuwa wakati umefika kwa
halmashauri kuweza kuyaainisha maeneo yote muhimu yenye fursa mbalimbali za
biashara na uwekezaji.
“Mkutano huu na wadau wote wa baraza ambao
unawajumuisha wajumbe kutoka halmashauri zote za mkoa huu ni vyema mnapo rudi
kwenye maeneo yenu ya kazi mkafanya mnyakato wa kuainisha fursa zote,”
alisisitiza Bw. Mbilinyi.
Alisema baraza linaamini endapo
halmashauri zitaibua fursa za biashara mapato ya serikali yataongezeka pia
ajira kwa vijana zitaimarika hivyo kipato kwa watanzania kitakua pia.
aliwambia waandishi wa habari mkoani humo
muda mfupi mara baada ya kumalizika kwa kiako cha baraza la biashara la mkoa wa
ruvuma kuwa vivutio vingi katika sekta za utalii, kilimo na madini,
vinaweza kuubadilisha taswira ya mkoa wa huo kwa kipindi kifupi.
“Huu mkoa unakila sababu za kujivunia
katika uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara kwani una ardhi ya
kutosha yenye rutuba na mvua ya kutosha pia,” alisema na kusisitiza kuwa hivyo
vyote vitumike kubadilisha maisha ya watu na kukuza kipato.
Alisema mbali na Kilimo, Mkoa wa Ruvuma
una madini ya Uranium, makaa ya Mawe na maeneo mazuri ya
kuvutia utalii wa ndani na nje ya nchi.
“ Mkoa huu ni tajiri sana, kila kitu
kipo jambo kubwa ni kwa watendaji wa halmashauri kuweka mazingira
mazuri ya kufanya biashara na kuvutia zaidi uwekezaji katika sekta
mbalimbali za kiuchumi na kubadilisha maisha ya watu,” alisema
Alisema kuwepo kwa baraza la mkoa ambalo
linajuisha wajumbe kutoka sekta za umma na binafsi litakuwa chachu
kubwa ya kuongeza kasi ya kimaendeleo katika wilaya zote mkoani hapa.
“Kikao hiki kitakuwa ni mwongozo tosha
katika kuwekana sawa , tumejadili mambo mengi ya msingi na pia naamini kuwa
baada ya muda mfupi kutakuwa na matokeo mazuri,”alisisitiza.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Nyasa
Ernest Kahindi, alisema wilaya yake inategemea sana uvuvi ili kuingiza kipato
katika halmashauri hiyo na kusema kuwa lengo lao kwa sasa ni kuwawezesha vijana
kwa kuwapatia zana za kisasa za kuvulia samaki.
“Vijana wetu wamekuwa wakitumia uvuvi wa
kienyeji sana lakini kwa sasa tumeagiza boti za kisasa ili waweze kuvua kisasa
zaidi,” alisema
Ameongeza kuwa walikuwa wanatumia mitumbwi
jambo ambalo lilikuwa linahatarisha maisha yao, kutokana na kutokuwa na uimara
na viwango vya kutosha wawapo ziwani.
“ Kwa kweli tumefanikiwa katika hili
vijana pamoja na akina mama waliokuwa wanasumbuka watakuwa salama na kipato
kitaongezeka katika kaya,” alisema Kahindi
Nae mwenyekiti wa chama cha wenye viwanda
biashara na kilimo ( TCCIA) wilaya ya Tunduru Mohamed Kiondo alisema Baraza
hilo limewapa mwanko katika kuhimiza suala la kilimo katika wilaya zao, kwani
ndio kitu pekee kitakachomkombo mwananchi wa Ruvuma.
“Mkoawetu uantegemea kilimo, tuna tumbaku,
korosho pamoja na zao la mahindi haya ni mazao makuu na yanaingiza pesa nyingi,
baraza hili I fursa pekee ya kujitangaza,” alisema Kiondo.
Aliongeza kuwa yanayojadiliwa katika vikao
vya mabaraza ya mikoa pamoja na wilaya yanatakiwa kufanyiwa tathimini ya hali
ya juu ili kuleta matokeo chanja katika kukuza uchumi wa mkoa na taifa kwa
ujumla.
Mwisho
No comments:
Post a Comment